Header Ads Widget

HIFADHI YA TAIFA YA ARUSHA YATUMIA PICHA YA MNYAMA MBEGA KAMA NEMBO YA HIFADHI HIYO


Na,Jusline Marco:Arusha

HIFADHI ya Taifa ya Arusha imeendelea kuwa kivutio muhimu cha utalii nchini, huku idadi ya watalii wanaotembelea eneo hilo ikiongezeka kutokana na vivutio vya kipekee vinavyopatikana ndani ya hifadhi hiyo.

Hifadhi hiyo inayosimamiwa na Tanzania National Parks Authority (TANAPA) ipo umbali wa takribani kilomita 30 kutoka Arusha, na imekuwa ni lango la watalii kuweza kuingia katika hifadhi nyingine kutokana na hifadhi hiyo kuwa karibu na uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Miongoni mwa vivutio vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ni pamoja na Mlima Meru, ambao ni mlima wa pili kwa urefu nchini baada ya Mlima Kilimanjaro,Creta/kasoko ya Ngurudoto,Ziwa Momela,Eneo la Serengeti ndogo,Mkuyu wenye pango,Njia aliyopita Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akitengeneza Movie ya Amaizing Tanzania,Kaburi ya mwanamke muwindaji wa kwanza Duniani Dkt. Magreth Trape.



Pamoja na vivutio hivyo Mnyama aina ya mbega ambaye kwa kitaalamu anafahamika kama black and white Colobus monkey ndiye mnyama pekee katika Hifadhi ya Taifa ya Arusha ambaye anatumika kama nembo kwani ni alama ya kipekee inayobeba maana kubwa ya uhifadhi wa wanyamapori na utambulisho wa hifadhi hiyo na ni miongoni mwa wanyama wanaopatikana kwa wingi ndani ya hifadhi ya Arusha.

Katika maelezo yake kwa waandishi wa habari Afisa Mwandamizi wa Uhifadhi kitengo cha Utalii ANAPA,Jerome Boniface Ndanzi, amesema nembo hiyo huwakilishwa kama ishara ya uhai wa misitu ya milimani inayopatikana ndani ya hifadhi, hasa katika maeneo ya Mlima Meru ambapo Mnyama huyo huishi juu ya miti mirefu, jambo linaloonyesha umuhimu wa kulinda misitu kwa ajili ya kuendeleza makazi yake na viumbe wengine.

Kutokana na upekee wake mnyama huyo ni ishara ya amani na utulivu, kwani mbega si mnyama mkali bali huishi kwa makundi kwa utulivu mkubwa na anawakilisha bioanuwai ya hifadhi, akionyesha kuwa eneo hilo lina viumbe mbalimbali wanaohitaji kulindwa ambapo nembo pia inaunganisha ujumbe wa Tanzania National Parks Authority (TANAPA) wa kulinda na kuhifadhi rasilimali za asili kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI