Header Ads Widget

ETHIOPIA YAWAKAMATA WATU 658 KWA KUHUSIKA NA BIASHARA HARAMU YA MAFUTA

 

Watu 658 wamekamatwa nchini Ethiopia, wakiwemo maafisa wa serikali, wanaoshukiwa kujihusisha na biashara haramu ya mafuta na kuhodhi bidhaa hiyo muhimu wakati nchi inakabiliwa na uhaba kutokana na vita vya Iran, gazeti la kibinafsi la Addis Standard linaripoti.

Waziri wa Biashara Kasahun Gofe alisema kuwa kukamatwa kwa watu hao ni sehemu ya hatua za kiutendaji zilizoimarishwa chini ya kikosi kazi kipya kilichopewa jukumu la kufuatilia usambazaji wa mafuta kote nchini.

Kasahun alionya kuwa usambazaji wowote wa mafuta nje ya mfumo uliowekwa utachukuliwa kuwa kinyume cha sheria na yeyote atakayepatikana na hatia atakabili na adhabu kali, huku mamlaka ikiendelea na juhudi za kudhibiti biashara haramu ili kuleta utulivu wa soko.

Wakati huo huo, waziri huyo alisema kuwa wasambazaji wa mafuta katika eneo la Mashariki ya Kati wameshindwa kuwasilisha tani 180,000 za mafuta nchini Ethiopia wakati wa vita.

Kulingana na ripoti hiyo, mamlaka ilikuwa imenasa zaidi ya lita 720,000 za mafuta, na kuirejesha katika udhibiti wa serikali wakati vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran huku usambazaji wa dizeli ya kila siku ya Ethiopia ikipunguzwa kutoka lita milioni 9.2 hadi milioni 4.5.

MWISHO.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI