Header Ads Widget

TRUMP: 'HAKUNA NJIA NYENGINE ISIPOKUWA KUAHIRISHA MKUTANO WANGU NA CHINA

 

Donald Trump na Xi Jinping

Rais Trump alisema Jumatatu kwamba anapanga kuchelewesha ziara ya China baadaye Machi kwa takriban mwezi mmoja kwa sababu ya vita vya Iran.

"Ni rahisi sana. Tuna vita vinavyoendelea. Nadhani ni muhimu kuwa hapa," alisema, akisisitiza "hakuna hila" na alikuwa akitarajia kumuona Rais Xi Jinping.

Hatua hiyo inakuja siku moja baada ya Trump kuliambia gazeti la Uingereza la Financial Times kwamba anaweza kuahirisha mkutano huo ikiwa China haitasaidia kufungua mlango wa bahari wa Hormuz - njia muhimu ya maji kwa usafirishaji wa mafuta .

Matamshi hayo ya Trump yanakuja huku msuguano kati ya mataifa hayo mawili yenye uchumi mkubwa zaidi duniani ukizidi kuchochewa na vita vya Iran.

Beijing ni mnunuzi mkuu wa mafuta ya Iran na imekosoa mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya nchi hiyo.

Washington pia ilitangaza kuwa itachunguza mazoea ya biashara kati ya orodha ya nchi, pamoja na Uchina, baada ya sera ya ushuru ya Trump kutupiliwa mbali na Mahakama ya Juu mnamo Februari.

Wawakilishi kutoka Marekani na China wamekutana mjini Paris katika siku za hivi karibuni kwa mazungumzo kuhusu uwekezaji, ushuru na vikwazo vya kiuchumi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI