Katika wiki iliyopita, na tena mapema hii leo, Rais wa Marekani Donald Trump amesema alitaka kuchangia katika uteuzi wa kiongozi mpya mkuu wa Iran.
Ingawa aliashiria kwamba angekuwa wazi kwa mtu anayehusishwa na uongozi wa zamani kuchukua madaraka, alipinga peupe mtu huyo kuwa Mojtaba Khamenei - ambaye amethibitishwa tu kuwa mrithi wa baba yake.
"Mtoto wa Khamenei simkubali," Trump alisema mapema wiki hii. Na saa chache tu zilizopita, alisema kwamba, bila idhini yake, Yeyote atakayechukua nafasi hiyo "hatadumu kwa muda mrefu".
Israeli ilitoa onyo kabla ya mtoto wa pili wa Khamenei kuthibitishwa kuwa kiongozi mkuu mpya - ikisema kwamba "itaendelea kumfuatilia kila mrithi" wa marehemu Ayatollah.





0 Comments