![]() |
| Dkt. Janemary Ntalwila |
Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani, tarehe 08 Machi, Mwaka huu.
Mwanasayansi Mwanamke anaijulisha jamii kunauwezekano wa Maisha jumuishi kati ya binadamu na wanyamapori huku Swali linabaki inawezekana vipi binadamu kuishi pamoja na mnyamapori mkali ?
Huyu ni Dkt. Janemary Ntalwila mtafiti Mkuu kutoka TAWIRI na mbobezi katika utatuzi wa migongano baina ya binadamu na wanyamapori wakali na waharibifu.
Dkt. Ntalwila anabainisha kuwa sayansi ni dira ya Maisha jumuishi kati ya binadamu na wanyamapori kama vile tembo,mamba, kiboko, Simba nk ambapo anabainisha tafiti zimesaidia ahueni kwa wananchi waliokuwa wakipata usumbufu na uharibifu wa tembo, mamba na viboko
Akigusia changamoto ya Mamba na viboko inayoathiri wananchi waishio pembezoni mwa mito/maziwa Dkt.Ntalwila amesema TAWIRI kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imekuwa mstari wa mbele katika ujenzi wa vizimba maalumu vya kudhibiti athari za mashambulio ya Mamba na Viboko sambamba na kutoa elimu ya kutumia vizimba hivyo kwa wananchi husika.
Aidha, amehitimisha kuwa utafiti wa kisayansi umesaidia kurejea kwa hali ya usalama wa maisha ya kila siku kwa wananchi waishio pembezoni mwa mito/maziwa kuendelea na utamaduni na shughuli zao bila athari za mashambulio ya mamba ambapo hadi sasa serikali imewezesha ujenzi wa vizimba zaidi ya 50 katika maeneo yaliyoathirika zaidi: ziwa Victoria, Tanganyika, Nyasa na mito mikubwa ikiwemo Ruvu, Pangani, Kilombero, Ugalla ,Ruvuma n.k.
Ujenzi huu uneenda sambamba na kutoa elimu kwa wananchi wa eneo husika namna ya kutumia na kutunza vizumba hivi.
![]() |
| Dkt. Janemary Ntalwila akiwa 'field' uwekaji wa vizimba vya kuzuia mamba |








0 Comments