Header Ads Widget

BIBI MIAKA 70 AFARIKI KILOSA KWA KUSOMBWA NA MAJI, JUHUDI ZA KUREJESHA MAWASILIANO ZAENDELEA.

 


Na Lilian Kasenene, Morogoro-Matukio DaimaApp

MVUA zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini na kusababisha mafutiko yakiwemo ya wilaya ya Kilosa Morogoro zimesababisha athari ya uharibifu wa  miundombinu, makazi ya watu kujaa maji, pamoja na kifo  kimoja cha mama mwenye umri wa miaka 70  eneo la Kidete Stesheni  alipokuwa kwenye jitihada za kuvuka Mto Mkondoa.


Mkuu wa wilaya ya Kilosa , Shaka Hamdu Shaka alisema hayo juzi mjini Kilosa kuwa mvua kubwa zilizonyesha Machi 9, mwaka huu zilileta athari maeneo ya  Miyombo , Mhenda na Mkata Stesheni  zilizopo wilayani humo.


Shaka alisema kwa haraka na  tathimini iliyofanyika  kuna baadhi ya makazi ya watu yameathirika kwa kiasi kikubwa  ambapo eneo la Miyombo zaidi ya nyumba 100 zimeathirika kwa kuungiliwa na maji ya mafuriko ya mvua.



Shaka alisema kwa  upande Miyombo kwa sasa mawasiliano yamefunguka hadi kufika eneo la Muhenda jambo kunahitajika ukarabati mkubwa wa  barabara kutoka  Kilosa- Muhenda  kwa vile  athari yake ni kubwa.


Pia alisema mafuriko hayo aliathiri eneo la Mkata Stesheni ambapo kwa siku ya juzi barabara ilifunga kabisa ingawa kwa sasa imeanza kupitika kwa tofauti na siku ya kwanza .


“ Kwa siku ya mafuriko hayo njia ilikuwa haipitiki  ilikuwa lazima uzunmguke  hadi Dumila – Mvomero , Morogoro na ndipo uende  Mikumi “  alisema Shaka.


“ Kwa sasa tumekuwa na  hofu ya m to Mkondoa kwa sababu maji ni mengi na endapo kina cha maji kikiongezeka kidogo kuna hatari ya maji kwenda kwenye makazi ya wananchi “ alisema Shaka


Mkuu wa wilaya alisema kutokana ana hali hiyo, Taasisi zinazohusika zitaweza kufika eneo la mto mkondoa ili kuona namna ya kuchukua jitihaza za haraka  na za dharua.


Wakati huo huo, Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Adam Malima aliyetembelea eneo Barabara Mikumi – Ifakara  baada ya Daraja namba nne  lililopo eneo la Mikumi kukatika usiku Machi 9, 2026  na kusababisha adha kwa wananchi na huduma za usafiri.


Malima, akiwa katika eneo hilo aliwataka  wananchi na watumiaji wa barabara hiyo kuwa na subira wakati Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kurejesha mawasiliano hayo.



Malima aliwataka wataalaamu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) mkoa wa Morogoro  kufanya kazi usiku na mchana ili kurejesha mawasiliano ya eneo hilo kwa haraka.


Malima alimwagiza Meneja wa TANROADS wa Mkoa huo kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi wake katika daraja hilo lililokatika.


“ Kwa sasa jitihada zinazofanywa na serikali ni kuimarisha kwa haraka eneo mojawapo ili kurahisisha wananchi kupita na ninawasii  wenye magari makubwa kuwa na subira hadi hapo wataalamu watakapojiridhisha kutengemaa kwa Daraja hili” alisema Malima.


Mkuu wa mkoa huyo pia waliwaagiza wahansidisi wa Wakala huo kuwa na  utaratibu wa kukagua madaraja mara kwa mara ili kuyafatia ukarabati na  kunusuru maisha ya watu na mali zao.



Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa huo , Mhandisi Patrick Rambika, alisema athari hizo zilitokea usiku wa kuamkia Machi 9, 2026 na kuharibu madaraja hayo kukatika na kuleta athari ya  usafiri na usafirishaji kwa maeneo ya Mikumi- Ifakara na kusitishwa kwa muda.


Nao baadhi ya wananchi na watumiaji wa barabara hiyo wameiomba Serikali kusaidia matengenezo ya barabara hiyo kukamilika mapema, kwa kuwa ni kiungo muhimu cha usafiri na usafirishaji wa bidhaa mbalimbali ndani nan je ya Mkoa wa Morogoro.


Mwisho.





Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI