Gari lililoharibiwa katika mashambulizi ya Marekani nchini Venezuela.
Serikali ya Cuba inaripoti kuwa raia 32 wa Cuba walikufa katika mashambulizi yaliyofanywa na vikosi vya Marekani nchini Venezuela mapema Jumamosi asubuhi, ambapo Rais Nicolás Maduro na mkewe Cilia Flores walikamatwa.
"Kutokana na shambulio la kihalifu lililofanywa na serikali ya Marekani dhidi ya taifa la Venezuela, (...) Wacuba 32 walipoteza maisha katika mapigano, serikali ya Rais Miguel DÃaz-Canel ilisema.
DÃaz-Canel alitangaza siku mbili za maombolezo kwa heshima ya Wacuba waliouawa wakati wa operesheni ya vikosi vya Marekani.
Kabla ya taarigfa hii kutokea, Waziri wa Ulinzi wa Venezuela, Jenerali Mkuu Vladimir Padrino López, alikuwa ameripoti kwamba walinzi wengi Maduro "waliuawa" na jeshi la Marekani ambalo lilimkamata mtawala wa Venezuela na mkewe.
Maduro anatarajiwa kufikishwa mahakamani nchini Marekani leo.





0 Comments