Na Hamida Ramadhan, Matukio Daima Media Dodoma
MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, ametoa wito kwa wananchi na viongozi wa dini kuhakikisha maombi yanawekwa mbele na kila mmoja anatimiza wajibu wake katika kulinda amani ya nchi, hasa katika kipindi hiki ambacho zimekuwepo taarifa za uwezekano wa machafuko kuelekea Desemba 9.
“Kila mmoja ana wajibu wa kulinda amani wakati huu si wa kusubiri tu tarehe 9 itakuwaje hatupaswi kulala leo ili kuhakikisha kesho kunakuwa na salama,” amesema Senyamule akisisitiza umuhimu wa kila mwananchi kuchukua hatua.
Ameongeza kuwa viongozi wa dini wana nafasi ya kipekee katika kuhamasisha umoja, maelewano na kutuliza mioyo ya wananchi, hasa kipindi hiki ambacho kumekuwa na taharuki katika maeneo mbalimbali.
“Huu si wakati wa kulala usingizi huu ni wakati wa kushikana na kuzungumza lugha ya amani tukifanya hivyo, tutakuwa tumetimiza wajibu wetu,” amesema.
Akizungumza leo wakati wa kufungua kikao maalumu cha maombi kilichowakutanisha viongozi wa dini katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Senyamule alisema Serikali imeweka siku tatu Desemba 7, 8 na 9 kuwa za maombi ya kuombea utulivu na mshikamano wa taifa.







0 Comments