Header Ads Widget

POLISI YAMSHIKILIA MWANAMKE ALIYEUA MWANAE KWA KIPIGO


Na  Matukio Daima  App

 Mbeya 

MWANAMKE Mmoja  aitwaye ,Marry Timotheo mkazi wa kijiji cha Garijembe kata ya Tembela Wilaya ya Mbeya anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga na kitu kizito kichwani mtoto wake ,Scola Mwaba(10)kwa madai ya kuzidi utukutu kisha mwili wake kutupa shamba lilo karibu na nyumbani anakoishi .

Akizungumzia tukio hilo Desemba 10,2025 Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema marehemu Scola alikuwa Mwanafunzi wa Darasa la Nne shule ya Msingi Ngonde wilaya ya Mbeya. 

Kuzaga amesema kuwa tukio hilo limetokea Desemba 9,2025 ,majira ya saa 6.30 mchana katika Kijiji cha Garijembe ,Kata na Tarafa ya Tembela  Wilaya ya Mbeya.

"Mama wa marehemu alimshambulia kwa kitu kizito kichwani  mtoto wake kwa madai ya kuzidi utukutu kisha mwili wake kutupa jirani na shamba la nyumba anakoishi "amesema Kamanda Kuzaga. 

Aidha Kuzaga ameeleza kuwa pia licha ya  kumshikilia mama wa marehemu ,pia  jirani yake ,Sharifa Nzalanje anashikiliwa na Polisi baada ya kuhusika  kushirikiana katika tukio hilo.

 Hata hivyo amesema kuwa  uchunguzi  wa awali umebaini chanzo cha tukio hilo ni kujichukulia sheria mkononi kumuadhibu marehemu kwa kumpiga  hadi kufa na kisha mwili wake kutupa shambani jirani na nyumba wanaoishi. 

Kuzaga amesema kuwa baada ya kubaini  kuwa  marehemu amefariki dunia  mama mzazi kwa kushirikiana na jirani yake walienda kutupa mwili wake shambani .

Amesema kuwa watuhumiwa  wanaendelea kushikiliwa  na upelelezi ukikamilika  hatua za kisheria  zitachukuliwa.

Kamanda Kuzaga ametoa  wito kwa  wazazi  na walezi kuacha  vitendo vya kujichukulia sheria mkononi kwa kuadhibu watoto badala yake watoe adhabu za kuwarekebisha  kuwafundisha mienendo ya maadili mema.

Pia amezitaka jamii kuwa mabalozi wa kutoa taarifa za wazazi na walezi wanaofanya vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ili hatua za kisheria zichukuliwe na kuhepuka madhara yanayoweza kuwapata ikiwepo kupoteza maisha au ulemavu wa kudumu.

Fatuma Idrisa ni mkazi Inolo wilaya ya Mbeya amesema kuwa ipo.haja kwa wazazi  na walezi kuacha kutumia vipigo vilivyo pitiliza kwa watoto wao pindi wanapokuwa na changamoto za kifamilia hivyo hasira kumalizia kwa watoto.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI