Vijana wamehamasishwa kuwa mstari wa mbele katika kukemea maovu na kulinda amani na utulivu uliopo nchini pamoja na kujiepusha na makundi yenye kutenda Vitendo visivyokubalika kisheria na vyenye kuhatarisha amani ya Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa kufuatia matukio ya uvunjifu wa amani yaliyojitokeza kwenye Miji mbalimbali ya Tanzania wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, suala ambalo limemlazimu Rais Samia Suluhu Hassan kuunda Tume maalum kufuatilia chanzo cha vurugu kutokana na kuwa tukio lililowagharimu wengi.
Akizungumza na waandishi wa habari, Bw. Hamis Jumanne, Mkazi wa Kichangani, Temeke amewaomba Vijana kuyakataa makundi yanayotishia amani ya Tanzania, akiwataka kutumia muda wao mwingi kujiendeleza kiuchumi badala ya kutumika kuharibu amani.
Jumanne amesisitiza kutafuta namna nzuri ya kushughulikia matatizo na mapungufu yaliyopo kwa namna ifaayo na isiyoharibu tunu za Taifa, akihimiza mazungumzo zaidi kati ya wananchi na Viongozi katika kutatua kero zilizopo.






0 Comments