Header Ads Widget

SIRRO AHIMIZA ELIMU YA COMPUTER KWA WANAFUNZI WA VYUO

 

Na Fadhili  Abdallah,Kigoma

MKUU wa mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro amewataka wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya kati  mkoani Kigoma kuongeza kasi katika kujifunza computer na matumizi sahihi ya vifaa hivyo kwani vina mchango mkubwa katika maisha yao ya baadaye

Balozi Sirro ametoa rai hiyo akikabidhi sehemu ya computer 50 kwa chuo cha ufundi Stadi (VETA) Kigoma ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake kwa chuo hicho alipofanya ziara chuoni hapo na kukuta uwepo wa changamoto wa vifaa hivyo katika kujifunza na kufundishia.

Mkuu wa mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro akikabidhi sehemu ya Computer 50 alizoahido kutoa kwa Chuo Cha Ufundi Stadi (VETA) Kigoma

Mkuu huyo wa mkoa Kigoma alisema kuwa kwa sasa dunia imeelekea katika matumizi ya Computer kwa sehemu kubwa ya maisha ya binadamu, shughuli za utendaji na mipango ya maendeleo na kwamba matumizi sahihi ndiyo yatayowavusha vijana katika mipango yao ya maendeleo. 

Aidha Mkuu huyo wa mkoa amevitaka vyuo vya kati vya elimu mkoani Kigoma kusisitiza ufundishaji elimu ya Computer kuwezesha wahitimu wa vyuo hivyo kuwa na uelewa wa juu wa matumizi ya vifaa hivyo ili kuwasaidia katika shughuli zao mbalimbali baada ya kumalizi masomo.


                        Mkuu wa Chuo cha ufundi Stadi VETA Kigoma, Paul Kimenya

Akizungumza baada ya kupokea Computer hizo Mkuu wa chuo cha VETA Kigoma, Paul Kimenyi alisema kuwa kutolewa kwa vifaa hivyo kutachochea na kurahisisha ufundishaji akikiri kuwepo kwa changamoto ya upungufu wa vitendea kazi hivyo ukilinganisha na idadi ya wanafunzi na masomo yanayofundishwa.

                   Amani Chaulaya Rais wa serikali ya wanafunzi VETA Kigoma

Kwa upande wake Raisi wa  serikali ya wanafunzi wa Chuo cha VETA,Kigoma, Amani Chaulaya alisema kuwa upungufu wa vifaa kwa ajili ya kujifunzia imekuwa ni changamoto na kwamba kutolewa kwa computer hizo kutawaongea mazingira mazuri ya kujifunza kwa kutumia teknolojia ya computer kwani masomo mengi sasa hivi chuoni hapo yanategemea uwepo wa vifaa hivyo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI