Na Fadhili Abdallah,Kigoma
MKUU wa mkoa Kigoma, Balozi Simon Sirro amewaonya watu wote wanaoijishughulisha na matukio ya ujambazi kwa kupora zana za wavuvi katika mwambao wa ziwa Tanganyika mkoani Kigoma ambapo ametangaza kuwa serikali imeanza kuchukua hatua kukabiliana na hali hiyo.
Mkuu wa mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro (mwenye kofia kushoto) akitembelea na kukagua shughuli za uvuvi katika Mwalo wa Lubengera kijiji cha Msiezi wilaya ya Uvnza mkoani Kigoma ambapo pia alifanya mkutano wa hadhara na wananchi kufuatia matukio ya uporaji wa zana za uvuvi unaofanywa ziwa Tanganyika na kijiji kikiwa ni moja ya maeneo yanayokabiliwa na uporaji mkubwa wa zana hizo za uvuvi.
Balozi Sirro alisema hayo akizungumza na wananchi na wavuvi wa Mwalo wa Lubengera kijiji cha Msiezi wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma alipotembea mwalo huo kukagua na kuzungumza na wananchi wa vijiji vya mwambao wa ziwa Tanganyika akieleza hatua ambazo serikali imeanza kuchukua kukabiliana na hali hiyo.
Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa katika hatua za awali vikosi vya ulinzi na usalama ikiwemo polisi kikosi cha wana maji na jeshi la wananchi kikosi cha wana maji (Navy) watafanya doria ya pamoja katika mwambao wote wa ziwa Tanganyika kuhakikisha matukio ya uporaji wa zana za uvuvi mkoani humo hayatokei tena,
Mkuu wa mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro (kushoto) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Msiezi wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma akizungumzia masuala ya ulinzi na usalama wa ziwa Tanganyika kufuatia wimbi la uporaji wa zana za uvuvi katika mwambao wa ziwa Tanganyika mkoani Kigoma ambapo kijiji hicho kimeathirika kwa kiasi kikubwa na matukio hayo.




0 Comments