Header Ads Widget

MADEREVA WENYE PIKIPIKI ZA MKATABA WALIA NA VURUGU NA GHASIA ZA OKTOBA 29.


 Bwana Issa Salala, Afisa usafirishaji abiria kwa kutumia usafiri wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda anayefanya shughuli zake Jijini Dar Es Salaam ameeleza namna ambavyo ghasia, vurugu na maandamano ya Oktoba 29, 2025 yalivyomuingiza kwenye madeni makubwa yasiyolipika, kutokana na ghasia zile kuzuka wakati ambao hakuwa na akiba yoyote ndani kwake.

Salala amebainisha hayo wakati akizungumzia athari za ghasia na uharibifu wa Jumatano ya Oktoba 29, 2025 kwenye maeneo mbalimbali ys Mkoa huo, akisema suala hilo lilimfanya yeye kutotoka ndani zaidi ya siku tano, akiendesha pikipiki isiyokuwa yake, suala ambalo lilifanya aliyemkodishia pikipiki kudai malipo yake wakati alipokuwa amesimama kufanya kazi kutokana na vurugu hizo.

Aidha Salala amezungumzia pia mfumuko mkubwa wa bei uliojitokeza kutokana na uhaba wa bidhaa na huduma mbalimbali kwenye eneo lake, akisema Unga uliokuwa ukiuzwa Kilogramu moja shilingi 1,500 waliuziwa shilingi 4,000 huku Mchele wa Shilingi 2,000 kwa Kilo moja wakiuziwa zaidi ya shilingi 5,000.

"Ni muhimu kwasisi Vijana kufikiria mbele kabla hujafanya kitu, vijana walioandamana hawakufikiria matokeo ya baadae. Leo unga wa 1, 500 unaununua 4, 000, Mchele wa 2,000 unaunua 5,000 na kipindi hicho kuna zuio la kutotoka nje kutokana na usalama, sasa hela unatoa wapi? Tumeingia ndani nilikuwa mnene, tumetoka nimepungua kwani mwili umeisha huu sasa hivi." Amesema.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI