Header Ads Widget

LULIDA AUTAKA UMEYA MANISPAA YA LINDI




NA MATUKIO DAIMA MEDIA, LINDI 

Diwani Mteule wa Kata ya Mtanda Jimbo la Manispaa  kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Mheshimiwa Idd Lulida amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kugombea Nafasi ya Umeya Katika Manispaa hiyo


Fomu hiyo amechukua Leo November 20, 2025 Katika ofisi ya Chama Mkoa  zilizopo Wailes katika manispaa ya Lindi na kukabidhiwa fomu na Katibu wa chama hicho Wilaya ya Lindi bwana Mohammed Lawa 



Mhe Lulida amesema dhamira yake kuu ya kuomba ni kujielekeza katika kuboresha huduma muhimu za msingi kama elimu,barabara,afya na kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji sambamba na maandalizi ya kupokea miradi mikubwa ya kimkakati kama iliyoainishwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025-30 na kuitekeleza kwa pamoja kwa maendeleo ya Wananchi wa Manispaa ya Lindi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI