Header Ads Widget

WANANCHI MLENGE WAJITOKEZA KWA WINGI KUMSIKILIZA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI WILIAM LUKUVI

 WANANCHI wa kata ya Mlenge jimbo la Isimani wamejitokeza kwa wingi leo kusikiliza sera za mgombea ubunge wa jimbo hilo Wiliam Vangimembe Lukuvi.

Lukuvi amekuwa akipata mapokezi makubwa kwenye mikutano yake kila kata anayopita kuomba kura za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan  ,kura zake mbunge na kura za madiwani wa kata zinazounda jimbo la Isimani .

Akiwa katika mikutano ya kampeni Lukuvi amewaomba wananchi kuendelea kujenga imani na serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwani ni serikali yenye mapenzi ya kweli ya kuleta maendeleo na ndio maana wanashuhudia miradi mingi ikitekelezwa .

Lukuvi alisema ili miradi hiyo na mingine izidi kutekelezwa wananchi wanapaswa kutoa kura za kishindo oktoba  29 kwa Mgombea urais wa CCM Dkt Samia ,mbunge na madiwani wote wa CCM ili waweze kusimamia ilani ya CCM.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI