Header Ads Widget

WAKULIMA NJOMBE WAKIRI MBOLEA NI MSAADA MKUBWA KWENYE KILIMO

 

Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE 

 Wakati Tanzania ikiungana na mataifa mengine kusherekea siku ya Mbolea Duniani kila Oktoba 13 Ya Mwaka,Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea nchini TFRA  imesema Matumizi ya Mbolea tangu kuanzishwa kwa Ruzuku yameongezeka Toka Zaidi ya Tani laki Tatu Hadi Tani laki Tisa. 


Katika Kijiji Cha Ujindile kata ya Igosi wilaya ya Wanging'ombe mkoani Njombe kulikofanyika sherehe za siku ya Mbolea Kitaifa mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Bwana Joel Laurent anasema ongezeko Hilo limesaidia kuongeza tija kwenye chakula Hadi nchi kuwa  na Ziada ya chakula.

Baadhi ya wakulima wa viazi,Mahindi na Parachichi  wilayani Wanging'ombe akiwemo Elly Chengula,Shadrack Mligo na Israel Mwalongo wanasema  licha ya kukiri kusaidika na Mbolea za Ruzuku lakini uhaba wa maji umekuwa mwiba mkali kwao huku wakiomba kuchimbiwa visima katika Mashamba yao.  

Kwa Upande wake Ofisa Kilimo mkoa wa Njombe Wilson Joel anasema Matumizi ya Mbolea kwa wakulima imesaidia kuwa na Ziada ya chakula katika mkoa.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania TFRA Joel Laurent akiwa na mkulima wa Parachichi Ujindile Mzee Elly Chengula shambani kwake

Maadhimisho hayo yameenda sambamba na Kampeni ya kuwaelimisha wakulima juu ya Matumizi sahihi ya Mbolea kwa  Kauli mbiu ya Mali shambani,Silaha Mbolea.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI