Header Ads Widget

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO




Wananchi wa Mapinga Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani wamehamasika kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura kwenye uchaguzi Mkuu wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, wakihamasisha watanzania wote waliojiandikisha kwenye daftari la Mpigakura, kutumia haki yao ya Kikatiba kuweza kuchagua Viongozi sahihi watakaowaletea maendeleo.


"Tarehe 29 nitaamka asubuhi na familia yangu yote tutaenda kupiga kura na ninawasihi Watanzania wenzangu tutumie haki yetu ya Kikatiba na tujitokeze kwa wingi tukapige kura kuwachagua Viongozi tunaowataka na usipopiga kura utachaguliwa Viongozi usiowataka na matokeo yake ni malalamiko." Amekaririwa akisema Fatuma Mkumba, Mkazi wa Mapinga.


Wananchi hao kwa nyakati tofauti wakizungumza na Chombo hiki cha habari leo Jumatatu Oktoba 13, 2025 wamesisitiza pia umuhimu wa kila mmoja kupiga kura, wakisema Viongozi sahihi wanaochaguliwa na watu ndiyo wenye kuweza kuwaletea maendeleo katika ngazi mbalimbali na zaidi wakihamasisha kuchagua Viongozi kutokana na sera, ahadi na yale yote wanayoendelea kuyaeleza katika Mikutano yao ya Kampeni nchi nzima.


Kwa upande wake Bi. Tukae Rashid, Mkazi wa Mkoa wa Pwani amesisitiza pia umuhimu wa kuheshimu sheria na taratibu za uchaguzi, akiwashauri Wapigakura wengine kurejea majumbani na kwenye sehemu zao za kazi mara baada ya kumaliza kupiga kura badala ya kujiingiza kwenye Uvunjifu wa sheria ikiwemo kusalia Vituoni kulinda kura kama ambavyo baadhi ya wanasiasa na Vyama vya siasa vimekuwa vikishawishi wanachama wake kubakia Vituoni ili kulinda kura walizozipiga.


Tayari Rais wa Awamu ya sita ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya ulinzi na usalama amewahakikishia watanzania wotw utulivu, amani na usalama siku ya upigaji wa kura, akiwahimiza kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi hilo la kidemokrasia na kutotishwa na yeyote wakiwemo wale wanaohamasisha kufanya vurugu na maandamano wakati wa Uchaguzi huo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI