Header Ads Widget

WAHADZABE WA KARATU WAISUBIRI KWA HAMU OKTOBA 29

 

Jamii ya Wahadzabe wanaopatikana kwenye eneo la Mang'ola Wilayani Karatu Mkoani Arusha wameahidi kujitokeza kwa wingi kutimiza haki yao ya Kikatiba ya kuchagua Viongozi katika uchaguzi Mkuu wa Jumatano ijayo Oktoba 29, 2025.

Wananchi hao wametoa kauli hiyo leo Jumatano Oktoba 22, 2025, wakiishukuru serikali pia kwa kuwakumbuka na kuwajumuisha katika zoezi hilo la Kikatiba licha ya kuishi kwao maeneo ya pembezoni na Jamii nyingine, wakisema wanatarajia kushiriki kwenye uchaguzi huo kikamilifu ili kuwachagua Viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo.
"Kwaniaba ya wenzangu Jamii ya Wahadzabe niwahakikishie kuwa tutaenda kupiga kura tarehe 29 na tutachagua Viongozi watakaoenda kutuangalia sisi kwa ujumla Wahadzabe wote ili tufanikiwe kimaendeleo kwasababu sisi tunaishi porini na hatujui mengi yanayoendelea kwahiyo tutawachagua wanaoweza kutuletea maendeleo huku." Amesema mmoja wa wananchi wa Jamii hiyo.

Kwa upande wao Ruben Mathayo, Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Tanzania na Mariam Anyanyire, Mhamasishaji ndani ya jamii hiyo, wameeleza kuwa muamko ni mkubwa kwa jamii hiyo kuelekea uchaguzi Mkuu wakiahidi kuwa kila mwenye haki na sifa ya kupiga kura atajitokeza siku hiyo kuwachagua Viongozi wanaowataka.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI