Header Ads Widget

UMOJA WA AFRIKA WAMKUMBUKA ODINGA

 

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC), Mahmoud Ali Youssouf, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha mwanasiasa wa upinzani Kenya, na Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri hiyo, Raila Amolo Odinga

Kwa niaba ya Umoja wa Afrika, vyombo na taasisi zake, mwenyekiti huyo ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Odinga, Serikali na wananchi wa Kenya, na na Afrika nzima inayoomboleza msiba huu mkubwa.

Amemtaja Odinga kama mtu mashuhuri katika maisha ya kisiasa na mpiganaji thabiti wa demokrasia, utawala bora na maendeleo yanayozingatia watu na ameacha alama isiyofutika sio tu kwa Kenya bali katika bara zima la Afrika.

Mwenyekiti Youssouf anasema, "Afrika imepoteza mmoja wa wanawe wenye maono; kiongozi aliyejitolea maisha yake kutafuta haki, demokrasia na umoja. Urithi wake utaendelea kujenga Afrika yenye amani, ustawi na demokrasia."

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI