Header Ads Widget

RAIS WA ZAMANI WA UFARANSA AFUNGWA MIAKA MITANO

 

Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy, ameanza rasmi kutumikia kifungo cha miaka mitano gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kula njama ya kufadhili kampeni zake za urais mwaka 2007 kinyume cha sheria.

Mahakama imethibitisha kuwa fedha zilizotumika kufadhili kampeni hizo zilikuwa zikitoka kwa aliyekuwa kiongozi wa Libya, marehemu Muamar Gaddafi.

Sarkozy mwenye umri wa miaka 70, anatarajiwa kutumikia kifungo chake katika Gereza la La Sante lililopo jijini Paris.

Hata hivyo, kiongozi huyo wa zamani ameendelea kukanusha madai hayo, akisisitiza kuwa hajawahi kujihusisha na uhalifu wowote unaohusiana na uchaguzi huo.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI