Na Shemsa Mussa -Matukio Daima
Kagera.
Katika kuadhimisha miaka 25 ya huduma kwa wakulima na wafugaji, PASS Trust imeandaa jukwaa maalum kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na taasisi za fedha nchini, ili kukuza upatikanaji wa mitaji kwa wadau wa sekta ya kilimo, uvuvi, mifugo na mazao ya misitu.
Akizungumza katika semina iliyowakutanisha wadau hao, Mkurugenzi wa Biashara wa PASS Trust, Bw.Adam Kamanda, amesisitiza umuhimu wa taasisi za kifedha kuendelea kushirikiana na PASS Trust katika kufungua fursa zaidi za uwezeshaji kwa wakulima, hususan wanaojihusisha na uzalishaji wa mazao ya Kanda ya Ziwa.
“Taasisi za kifedha zina nafasi ya kipekee katika kusaidia wakulima kuongeza tija na thamani ya uzalishaji. Kupitia ushirikiano na PASS, tunaweza kuwafikia wakulima wengi zaidi na kuwapa mitaji wanayohitaji kwa masharti nafuu,” amesema Bw ,Kamanda.
0 Comments