NA HADIJA OMARY
LINDI.....Mfuko wa hifadhi ya jamii NSSF Mkoa wa Lindi umezindua rasmi wiki ya huduma kwa wateja huku ikijivunia hatua kubwa waliyofikia Katika matumizi ya tehama ambayo yamerahisisha utoaji wa huduma kulingana na Kasi ya ukuwaji wa teknolojia duniani
Akizungumza wakati wa uzinduzi uliofanyika Katika ofisi za mfuko huo huko manispaa ya Lindi mkuu wa Wilaya ya Lindi victoria Mwanziva akatumia fursa hiyo kuwakumbusha waajiri kuhakikisha wanajiandikisha na kuwachangia wafanyakazi wao kwa mujibu wa Sheria
Amesema Mfuko huo umejidhatiti kuwafikia waajiri wote ambao hawajajiandikisha na kuwachykulia Hatua stahiki wale wote wanaolimbikiza michango ya wanachama
Kwa upande wake Meneja wa mfuko wa hifadhi ya jamii NSSF Mkoa wa Lindi Bwana Juma Namuna amesema toka mfuko huo umeaza kutumia mfumo wa Tehama wameweza kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wanachama wao
Amesema miongoni mwa manufaa wanayoyapata kutokana na mfumo huo ni pamoja na mfuko kuwawezesha wanachama kufungua madai ya mafao kwa njia ya mtandao ambapo imetoa fursa kwa wanachama walioko mbali na matawi ya mfuko huo kutolazimika kusafiri kufuata huduma hiyo
Wastaafu kuhakiki taarifa zao za mafao kwa njia ya mtandao , waajili kulipa michango Yao moja kwa moja kwa kutumia lango la waajiri (Employers portal)
" Kwa kupitia mfumo huu mwajiri pia anaweza malimbikizo yake ya michango na kuweza kupata namba ya malipo pasipo kulazimika kufika Katika Tawi la NSSF na hivyo kutoa muda wa uzalishaji"
Afisa wa hifadhi skimu kutoka NSSF bwana shabani haule akiwasihi wananchi ambao sio waajiria kujiunga na mfuko huo ili waweze kunufaika na mafao yanayotolewa na mfuko huo
0 Comments