Mwanamuziki maarufu wa muziki wa kufokafoka Sean "Diddy" Combs amemwandikia barua jaji anayesimamia kesi yake ya jinai, akiomba ahurumiwe wakati wa hukumu yake siku ya Ijumaa na kulaumu tabia yake ya zamani juu ya uraibu wa dawa za kulevya.
Katika barua hiyo yenye kurasa nne, Diddy anaomba radhi “kwa maumivu yote ambayo nimesababisha” na anasema kwamba amebadilika baada ya kukaa kwa miezi 13 katika jela ya Brooklyn.
Barua hiyo ya Alhamisi imetolewa saa chache kabla ya kusikilizwa kwa hukumu yake saa 10:00 ET (15:00GMT) siku ya Ijumaa.
Mnamo mwezi Julai, alipatikana na hatia ya mashtaka mawili ya ukahaba na sasa anakabiliwa na kifungo cha miaka 20 jela.
Waendesha mashitaka wanatafuta kifungo cha angalau miaka 11, lakini wanasheria wa Combs wanaomba kwamba aachiliwe baadaye mwezi.
0 Comments