Header Ads Widget

MUFTI ATAKA WAISLAMU KUZINGATIA MAFUNDISHO YA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29.

 


NA MATUKIO DAIMA MEDIA 

Mufti na Sheikh Mkuu wa Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Bin Zubeir Ally amewataka Waislamu na Watanzania kwa ujumla kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani na ustawi wa jamii hasa wakati huu ambapo Tanzania inaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.


Mbele ya waumini wa kiislamu Katika Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Mufti Sheikh Abubakar amesema amani ndiyo msingi wa uislamu na chachu ya maendeleo ya jamii yoyote ile, akisisitiza kuwa waislamu wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa katika kuhakikisha utulivu na mshikamano vinaendelea kuwepo.


"Maandishi yanasema wala msieneze katika nchi uharibu wowote wa kuweza kuleta matatizo. Je uislamu umezungumza amani? Niwaambie kuwa Msaafu mzima tukiufasiri ni amani, amani tupu, Mtume kipindi chote anazungumzia amani. Kipindi hiki tufundishe na tutangaze juu ya amani na mmomonyoko wa maadili." Amesisitiza kusema Mufti huyo.


Mufti pia ameeleza kuhusu umuhimu wa malezi ya watoto katika misingi ya dini, akieleza kuwa hilo ndilo jambo la msingi katika kukabiliana na mmomonyoko wa maadili unaozidi kushika kasi katika jamii, akitoa rai kwa wazazi na walezi kuwalea watoto wao kwa maadili ya dini na kulinda maadili ya Taifa kwa vizazi vijavyo.



Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Denis Masanja amewataka wananchi wote wa Wilaya hiyo wenye sifa na waliojiandikisha kwenye daftari na Mpigakura kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi wa Oktoba 29, 2025 ili kutimiza haki yao ya Kikatiba ya kupiga kura.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI