Header Ads Widget

MAOMBI YA DOTTO JASSON BAHEMU YATUA KWA RAIS DKT SAMIA.

NA MATUKIO DAIMA.

Mgombea Ubunge  Jimbo la Ngara kupitia Chama cha Mapinduzi CCM ndugu Dotto Jasson Bahemu amemuomba Dkt. Samia Suluhu Hassan mgombea nafasi ya  Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Kujenga kituo kipya cha Mabasi mjini Ngara. 

‎‎Dotto Jasson Bahemu ambaye ni  mgombea pekee wa Ubunge Jimboni la Ngara amewasilisha ombi hilo kwa niaba ya wananchi wa Ngara  kupitia mkutano wa Kampeni wa Mgombea nafasi ya Urais kupitia Chama cha Mapinduzi Dkt Samia Suluhu  uliofanyika Wilayani Karagwe.

‎Amesema, kujengwa kwa stendi mpya ya mabasi mjini Ngara kutachochea maendeleo ya Wilaya hiyo na kufungua fursa mbalimbali za biashara.‎

Katika hatua nyingine,amemueleza mgombea huyo ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Ngara ni moja ya wilaya zinazozalisha zao la Parachichi, kwa wingi.

Amemuomba Rais Dokta Samia Suluhu Hassan atakapopata ridhaa ya  kuchaguliwa, awasaidie wakulima kwa kuwajengea jengo maalum lenye vyumba vya  baridi (Cord Room) kwa ajili ya kuhifadhi  matunda ya Parachichi  kabla ya kusafirishwa.‎

Ombi lingine lililowasilishwa na Bahemu kwa Dkt. Samia ni ujenzi wa Barabara mpya ya Lami kutoka Nyakahura,kumubuga,Murusagamba,Keza Rulenge,hadi Murugarama, na Ujenzi wa mradi mpya wa maji kutoka mto Ruvuvu utakaogharimu kiasi cha Shilingi bilioni 41.

‎‎Mgombea huyo kijana wa Jimbo la Ngara amesema ikiwa maombi aliyowasilisha yatatekelezwa yataisogeza kasi ya kukua kwa uchumi na Maendeleo ya wananchi wa Wilaya ya Ngara inayopakana na nchi za Rwanda na Burundi 

MWISHO.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI