Header Ads Widget

KIFO CHA RAILA ODINGA :WABUNGE WASHINDWA KUJIZUIA BUNGENI

 

Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kimesababisha uchungu na simanzi kwa wafuasi wake na Wakenya kwa ujumla.

Raila alifariki siku ya Jumatano, Oktoba 15, alipokuwa akipatiwa matibabu nchini India.

Bungeni, wabunge wa ODM waliangua vilio baada ya kupokea habari hizo za kuhuzunisha.

Baadhi ya wabunge walitiririkwa na machozi na kushindwa kujizuia huku wakimsifu waziri mkuu huyo wa zamani.

Mwakilishi wa Kike wa Busia Cathrtine Omayo na Mbunge wake wa Likoni Mishi Mboko walishindwa kujizuia wakati taarifa za kifo cha Raila kilipotangazwa.

Wakenya wanaendelea kutoa heshima zao kwenye mitandao ya kijamii wakimkumbuka kwa namna mbalimbali.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI