Kwa mara ya kwanza katika karibu miaka 500 ya historia, Kanisa la Anglikana limemteua mwanamke kuliongoza.
Dame Sarah Mullally, 63, ameteuliwa kuwa Askofu Mkuu Mteule wa Canterbury.
Alikuwa akijenga msingi mpya katika taaluma yake aliyoichagua hata kabla ya kuwa kasisi.
Mwaka wa 1999 akawa afisa mkuu wa uuguzi mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kutokea nchini Uingereza.
Kwa zaidi ya miaka saba amehudumu kama Askofu wa London, mshiriki mkuu wa tatu wa makasisi katika Kanisa na mwanamke wa kwanza kufanya kazi hiyo.
Wanawake wameruhusiwa tu kuwa mapadri katika Kanisa la Anglikana tangu katikati ya miaka ya 1990.
Lakini kuna maaskofu wakuu katika Kanisa la Anglikana ambao wanapinga waziwazi wanawake kujiunga na ukasisi hata kidogo kuongoza taasisi hiyo.
Sheria inawahitaji Maaskofu Wakuu wa Canterbury kustaafu wakiwa na umri wa miaka 70, ambayo labda ni sababu mojawapo kwa nini wengine hawakumwona Dame Sarah Mullally akiwa na nafasi ya kuchaguliwa.
Hata hivyo ameishia kuandikisha historia. Tarehe ya kutawazwa kwakerasmi bado haijatangazwa.






0 Comments