Header Ads Widget

TRUMP ATANGAZA USHURU MPYA KWA BIDHAA ZINAZOINGIA MAREKANI

 

Ushuru wa Trump unashutumiwa

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza ushuru mpya kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka nje, ikiwemo dawa na malori.

Ametangaza kuongeza ushuru hadi asilimia 100 kwa dawa zinazotengenezwa nje kwa kutumia leseni za kampuni za Kimarekani, au zile zinazozalishwa ndani ya Marekani lakini kuuzwa kwa majina tofauti.

Hatua hii itaanza kutekelezwa kuanzia Oktoba 1, isipokuwa kwa kampuni zitakazojenga viwanda vya uzalishaji ndani ya Marekani.

Aidha, serikali ya Marekani imeweka ushuru wa asilimia 25 kwa malori makubwa ya kubeba mizigo, huku ushuru kwa vifaa vya jikoni na vya bafuni ukiongezwa kwa asilimia 50.

Rais Trump amesema kuwa hatua hiyo inalenga kulinda masoko ya ndani.

“Bidhaa nyingi kutoka nje zinaingizwa kwa bei ya kutupwa nchini mwetu, hali ambayo imeyasukuma bidhaa za ndani nje ya soko,” alisema kupitia ukurasa wake wa Truth Social.

Hata hivyo, hatua hiyo imezua pingamizi kutoka kwa wafanyabiashara wa Marekani, ambao wametoa wito kwa Ikulu ya White House kusitisha ushuru huo wa ziada.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI