Header Ads Widget

MWENYEKITI WA CCM TANGA AWATAKA WANACHAMA KUACHA MAKUNDI NA KUUNGANA KWA USHINDI WA KISHINDO.

 

NA AMINA SAIDI,TANGA,

Katika juhudi za kuimarisha umoja ndani ya Chama,Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Tanga Ustadhi Rajab Abdul Rahman,ametoa wito kwa wanachama na wagombea walioteuliwa kwenye kura za maoni kuachana na makundi yaliyojitokeza wakati wa mchakato huo,alisisitiza kuwa umoja ni nguzo kuu ya mafanikio pamoja na  ushirikiano utawawezesha kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu.

Kutokana na umuhimu wa kushinda uchaguzi,kauli hiyo aliitoa wakati wa mkutano wa pamoja na kamati za kampeni ngazi  ya Kata,Wilaya na Mkoa,Mwenyekiti huyo amesisitiza kuwa wanachama wanapaswa kuacha tofauti zao na badala yake waungane ili kuhakikisha chama kinaoata ushindi wa kishindo.


Kwa upande mwingine ,Ustadhi Rajab aliongeza kuwa chama kina msimamo thabiti dhidi ya wasaliti,Amesema wameamua kushirikiana na wanachama wote kwa lengo Moja la kuongeza idadi ya kura katika mkoa wa Tanga.

 Sambamba  na hayo alito wito kwa wale walioteuliwa kwenye nafasi ya kugombea ubunge au udiwani waache mara moja tambia ya kujitamba mbele ya wale wasioteuliwa ili kuacha kutengeneza makundi vivyohivyo na wale wasioteuliwa wanapaswa kuwa wavumilivu lakini pia kuficha hisia  zao ili Chama kisigawanyike.

Kwa upande wake mzee Musa Shekimweri ambaye alikuwa mwenyekiti mstaafu wa CCM Mkoa aliwataka wajumbe kuweza kutambua kuwa nafasi ya uchaguzi ni moja tu mtu anapoachwa kwenye kura au kutokuteuliwa ni kwaida wala sio jambo la kutengeneza  chuki na kipindi cha kura za maoni makundi pia kawaida ila baada ya hapo wanapaswa kukaa pamoja na kujenga  nyumba moja.

Alisema cha kufahamu ni kwamba wagombea wanaweza kujitokeza wengi kwenye kiti Kimoja lakini baada ya hapo  atakayekaa kwenye kiti ni mtu mmoja ambaye ndio atakayebahatika tu hivyo hakuna haja ya kugawanyika ndani ya Chama Cha mapinduzi. 

Hata hivyo alitoa ombi kwa viongozi wa CCM kuwa wakati wa Uchaguzi  tarehe 29 mwezi October  wale wazee wote ambao hawawezi kutembea na ni wapiga kura wafuatwe majumbani ila wafike kwenye vituo vya wapiga kura wapige kura zao kuwachagua viongozi wao.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI