Header Ads Widget

MASHINDANO YA MBIO ZA MAGARI AFRICAN RALLY KUFANYIKA MOROGORO KWA MARA YA KWANZA

 

Na Lilian Kasenene, Morogoro

Matukio DaimaApp 

MASHINDANO ya mbio za magari, African Rally championship kwa mara ya kwanza mkoani Morogoro yanatarajiwa kuanza sept. 19 hadi 21 mwaka huu 2025, ambapo hadi sasa washiriki 23 wameshajiandikisha.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa mashindano hayo msimamizi mkuu wa mashindano hayo Dk. Mosi Makau amesema maandalizi yamekamilika kwa asilimia 95.

Aidha Dk. Makau amesema maeneo yatakayotumika katika mashindano hayo ni shamba la miti la TFS na shamba la mkonge Tungi Manispaa ya Morogoro.

Hata hivyo Dk. Makau alisema kuwa baadhi ya washiriki wa mashindano hayo ya magari ni madereva wenye uwezo mkubwa zaidi na wanawania taji la Afrika.

kwa upande wake mwakilishi kutoka Mkwawa Leaf ambao ndio wadhamini wa mashindano hayo Emanuel Mhagama alisema kuwa kampuni yao inashirikiana na serikali kupitia wizara ya utamaduni sanaa na michezo katika kuhakikisha mashindano hayo yanakuwa na mafanikio.

Hata hivyo Mhagama alisema kuwa mashindano hayo yanawashirikisha washiriki wenye uzoefu mkubwa kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Uganda, Kenya, India na Burundi.

Aidha amesisitiza kuwa wao kama kampuni wako tayari kushirikiana ili kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa kiwango cha juu.


Naye Gwakisa Mahige ambaye ni mkuu wa ulinzi alisema kuwa ulinzi utaimalishwa kwa kiwango cha juu ili washiriki waweze kushiriki mashindano hayo kwa amani.

Aidha Mahige alisema kuwa maeneo yayakayofanyika mashindano hayo ulinzi utaimalishwa zaidi na hakutakiwa na muingiliano wowote wa vyombo vya moto kupita hadi muda wa mashindano utakapokwisha.

Mahige amewataka pia wananchi na mashabiki kufuata sheria na kanuni za mashindano hayo ili waweze kufurahia burudani hiyo ya mbio za magari.

Mahige pia amesisitiza kuwa mtu yeyote atakayevunja sheria kwa lengo la kuharibu mashindano hayo hatua kali zita hukuliwa dhidi yake.

Naye Satinder Birdi Mkurugenzi wa Magari ya Mashindano Tanzania , amethibitisha kuwa magari 23 kutoka mataifa mbalimbali yatashiriki, huku madereva na timu zao wakitarajiwa kuwasili nchini mapema wiki hii.

 Aidha amewataka mashabiki kusikiliza maelekezo watakayopewa ili kuweza kulinda usalama wao wakati wa mashindano hayo ya mbio za magari.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI