Header Ads Widget

DAWA MPYA YA KUPAMBANA NA VIRUSI VYA UKIMWI KUPATIKANA KWA BEI NAFUU

 

Dawa mpya ya kuzuia HIV itapatikana kwa gharama ya chini katika zaidi ya nchi 100 za kipato cha chini ndani ya miaka miwili, hatua inayotarajiwa kuwapa mamilioni ya watu fursa ya matibabu na uwezekano wa kuleta ulimwengu karibu na kumaliza janga la UKIMWI.

Dawa hiyo, iitwayo Lenacapavir na inayotolewa kwa njia ya sindano, inatazamiwa kuanza kutumika mapema mwishoni mwa mwaka huu, kwa gharama ya $28,000 (£20,000) kwa kila mtu kila mwaka.

Lakini tangazo la Jumatano linaahidi kupunguza bei hiyo hadi $40 pekee, karibu 0.1% ya gharama ya awali.

Toleo la bei ya chini litatolewa mwaka wa 2027 katika nchi 120 za kipato cha chini na cha kati.

Wanasayansi wanasema dawa hiyo huzuia virusi visijizalishe ndani ya seli.

Mpango huo wa kihistoria wa kutoa dawa za kupunguza makali ya virusi kwa watu wenye virusi vya Ukimwi katika nchi zinazoendelea ulisimamiwa na Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton baada ya mazungumzo na makampuni ya dawa.

Makubaliano hayo yaliyotangazwa Jumatano yalifikiwa kati ya Wakfu wa Clinton kwa ushirikiano na Gates Foundation na makundi mengine, ikiwa ni pamoja na taasisi ya utafiti ya Afrika Kusini, Wits RHI.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI