Waandamanaji wamekusanyika katika makutano na maandamano kote Israel asubuhi ya leo, wakishinikiza kusitishwa kwa kampeni ya kijeshi ya Israel huko Gaza na kurejeshwa kwa mateka waliosalia wanaoshikiliwa na Hamas.
Maandamano hayo yameandaliwa na Jukwaa la Hostages and Missing Families Forum - kundi ambalo kwa muda mrefu limeitaka serikali ya Israel kuweka kipaumbele cha kuachiliwa kwa mateka hao na kumaliza vita mara moja.
Kundi hilo pia linamtolea wito, tena, Rais Donald Trump kwa usaidizi wa kukamilisha makubaliano ya kusitisha mapigano na kuwarudisha nyumbani wale wote waliofungwa. Mateka 20 wanaoshikiliwa na Hamas bado wanaaminika kuwa hai.
Einav Zangauker, mama wa Matan Zangauker ambaye alitekwa nyara na Hamas tarehe 7 Oktoba 2023, amesema 'Netanyahu anaogopa jambo moja - shinikizo la umma’
"Kwa siku 690, serikali imekuwa ikiendesha vita bila lengo bayana," anasema wakati wa mkutano wa waandishi wa habari mjini Tel Aviv.
Picha zilizochapishwa mtandaoni zinaonyesha moto mkubwa ukiwashwa kwenye sehemu za barabara inayounganisha Tel Aviv na Jerusalem . Kwingineko, viungani mwa sehemu za Tel Aviv kando ya Barabara Kuu ya Pwani pia zimefungwa.
Maandamanao haya yanafanyika wakati Israel imekuwa ikiimarisha mashambulizi yake katika Ukanda wa Gaza, ikifanya mashambulizi katika mji wa Gaza kabla ya uvamizi wake uliopangwa katika eneo kubwa zaidi la mijini katika eneo hilo.
Israel imelaaniwa na watu wengi jana baada ya mashambulizi yake katika hospitali moja kusini mwa Gaza kuwaua takriban watu 20, wakiwemo waandishi wa habari watano na wahudumu wa afya wanne.
0 Comments