Header Ads Widget

AUSTRALIA YAILAUMU IRAN KWA MASHAMBULIZI YA CHUKI DHIDI YA WAYAHUDI SYDNEY NA MELBOURNE

 

Australia inasema itamfukuza balozi wa Iran baada ya kudai kuwa serikali ya nchi hiyo ilielekeza mashambulizi ya chuki dhidi ya Wayahudi huko Sydney na Melbourne.

Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema mashambulizi hayo ni "vitendo vya ajabu na vya hatari vya uchokozi vilivyopangwa na taifa la kigeni". Hakuna aliyejeruhiwa katika mashambulizi hayo yaliyotokea mwaka jana.

Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Australia (Asio) Mike Burgess amesema shirika lake lilikuwa na taarifa za kijasusi kwamba Iran "huenda" ilikuwa nyuma ya mashambulizi zaidi dhidi ya walengwa wa Kiyahudi katika matukio ya Australia.

Balozi Ahmad Sadeghi na maafisa wengine watatu wa Iran wameagizwa kuondoka Australia ndani ya siku saba. Iran bado haijasema lolote kuhusu tuhuma hizo.

Burgess alisema: "Iran imejaribu kuficha kuhusika kwake, lakini Asio anakadiria kuwa ilihusika na mashambulizi ya Lewis Continental Kitchen huko Sydney tarehe 20 Oktoba mwaka jana, na Sinagogi ya Adass Israel huko Melbourne tarehe 6 Desemba."

Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong alisema ni mara ya kwanza tangu Vita vya Pili vya Dunia kwamba Australia imemfukuza balozi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI