Header Ads Widget

TRUMP ASEMA HAKUNA MABADILIKO LAKINI 'WAMEPIGA HATUA KUBWA' BAADA YA MAZUNGUMZO NA PUTIN

 


Rais Donald Trump wa Marekani amesema yeye na Putin wamekuwa na mkutano wenye tija na kwamba wamepiga "hatua kubwa".

Trump na Putin walizungumza kwa pamoja jukwaani kwa takriban dakika 10. Wote wawili walionyesha ishara ya mazungumzo mema waliokuwa nayo wakati wa mkutano wao wa faragha, ingawa ulimalizika bila makubaliano madhubuti.

Putin alisema "ana nia ya dhati" katika kukomesha mzozo huo, ambao alielezea kuwa "janga".

Lakini alisema Urusi inahitaji "sababu za msingi" za mzozo huo zitatuliwe kwanza - na akaonya Ukraine na Ulaya hazipaswi "kuhujumu" mazungumzo hayo.

Putin, pia alielezea mkutano huo kama "mahali pa kuanzia kwa utatuzi" wa mzozo huku akisema uhusiano wake na Trump ni "imara" - na kukubaliana na madai ya mara kwa mara ya rais wa Marekani kwamba vita haingeanza ikiwa angesalia madarakani baada ya uchaguzi wa 2020.

Kwa upande wake, Trump alisema bado kuna mambo ambayo hawajakubaliana na "hakuna makubaliano hadi maafikiano yawepo" na kuongeza kuwa "hatukufikia" tulipotaka ila tumepiga hatua kubwa.

Trump alisema "wamekubaliana mambo mengi" lakini "machache" bado yamesalia, akiongeza kuwa "moja ni muhimu zaidi" bila kutaja hasa ni nini.

Trump alimalizia kwa kusema "kuna uwezekano mkubwa" ataonana tena na kiongozi wa Urusi hivi karibuni huku Putin akijibu kuwa: "Wakati ujao itakuwa Moscow"

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI