Header Ads Widget

NCAA KUSHIRIKIANA NA WIZARA ZA KISEKTA KATIKA KUHAKIKISHA KIJIJI CHA MSOMERA KINAKUWA KIJIJI CHA MFANO.


Na,Jusline Marco;Tanga

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) Abdul-razaq Badru amesema mamlaka hiyo itashirikiana na wizara za kisekta katika kuhakikisha kijiji cha Msomera Mkoani Tanga kinaendelea kuwa cha mfano kwa kuwekewa miundombinu yote wezeshi kwa ajili ya wananchi wanaohamia.


Akiwa na mwenyeji wake mkuu wa wilaya ya Handeni Salum Nyamwese,wakati alipotembea kijiji hicho kilichopo wilayani Handeni Mkoani Tanga, Kamishna Badru amejionea uendelezaji wa eneo hilo ambalo linatumika kwa ajili ya kuwamishia wananchi wa tarafa ya Ngorongoro wanaojiandikisha kuhama kwa hiari.

 


“Mheshimiwa mkuu wa wilaya kuna kazi kubwa ambayo serikali imefanya, tutaendelea kushirikiana katika kuhakikisha kijiji hiki kinakuwa bora  ili wananchi waliohamia na wale watakaohamia waweze kuishi hapa kwa furaha,”alisema Kamishna Badru.


Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Handeni Salum Nyamwese alisema kuwa kazi mbalimbali za uboreshaji wa miundombinu katika kijiji hicho zinaendelea ikiwa ni pamoja na ulinzi wa Nyumba ambazo zimeshakamilishwa kujengwa.

Kijiji cha Msomera kimekuwa ni kijiji cha mfano kutokana na serikali ya awamu ya sita kuamua kuweka miundombinu yote ya msingi ili wananchi wanaoishi katika eneo la Ngorongoro waweze kuhamia huko ili kupisha shughuli za uhifadhi katika hifadhi hiyo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI