Header Ads Widget

JESHI LA POLISI LATOA TAMKO KUELEKEA UZINDUZI WA KAMPENI KESHO

 


Na mwandishi wetu

Jeshi la Polisi nchini, limetoa tamko kuelekea uzinduzi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu zinazotarajiwa kuzinduliwa kuanzia kesho Agosti 28, 2025.

Akizungumza na waadishi wa  Habari Msemaji wa Jeshi la Polisi DCP David Misime amesema kuwa jeshi la polisi  lipo tayari na limejiandaa vizuri ipasavyo kuhakikisha linaendelea kuimarisha usalama wakati wote wa kampeni na baada ya kampeni.

“Jeshi la polisi Tanzania lingependa kuwafahamisha watu wote kuwa limejipanga vizuri kuendelea kuhakikisha usalama unaendelea kuwepo kabla ya kampeni na baada ya kampeni,Jeshi la polisi linatoa wito kwa wagombe na wadau wake wote kwa ujumla kukumbuka kuwa jukumu la kudumisha Amani,Utulivu na Usalama  ni letu sote kama watanzania na kamwe asiwepo mmoja wetu akawa chanzo cha kukiuka Sheria, Kanuni na Taratibu wakati wote wa kampeni na baada ya kampeni ili kuepuka vurugu au uhalifu wa aina yoyote ile kutokea.

Pia ameongeza kuwa kila mmoja anatakiwa azingatie  ratiba na muda wa kampeni aliopangiwa  ili kupunguza na kuepuka migongano kipindi ambacho kampeni hizo zitaanza.

“Pia kila mmoja wetu anatakiwa azingatie ratiba na muda wa kampeni aliopangiwa na  kuweza kufika katika eneo ambalo amepangiwa ili kuepuka migongano na mitafaruko au uhalifu wowote kuweza kutokea na sisi kama  jeshi la polisi hatutasita  kumchukulia hatua mtu yoyote atakayeonekana analengo la kuvunja Amani  kama seheria za Nchi zinavyoelekeza.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI