Shirikishi la Usalama wa Chakula (IPC) litatoa taarifa baadaye kuhusu njaa katika Ukanda wa Gaza.
Chombo kinachoungwa mkono na Umoja wa Mataifa kinachohusika na ufuatiliaji wa usalama wa chakula, ambacho chenyewe hakitangazi rasmi njaa, kilisema mwezi uliopita kwamba "hali mbaya zaidi ya njaa" ilikuwa "ikishuhudiwa Gaza".
Wizara ya Afya ya Gaza inayoendeshwa na Hamas inasema watu 271 wamekufa kwa "njaa na utapiamlo" tangu tarehe 7 Oktoba 2023 - ikiwa ni pamoja na watoto 112.
Mashirika ya kibinadamu yametoa wito kwa Israel kuwezesha upatikanaji wa misaada zaidi katika Ukanda huo, na kuonya uhaba wa chakula na maji unaweza kuibuka na kuwa baa la njaa kubwa.
Israel imekanusha kuwa Gaza kuna njaa, huku Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu akisema mapema mwezi huu kwamba "sera ya Israel wakati wote wa vita imekuwa ikizuia mzozo wa kibinadamu …".
Ripoti hiyo mpya inakuja chini ya saa 24 baada ya Netanyahu kusema kuwa ameidhinisha mipango ya shambulio kubwa katika mji wa Gaza, licha ya upinzani mkubwa wa kimataifa na wa ndani.
0 Comments