Header Ads Widget

TRAORE AIVUNJA TUME YA UCHAGUZI BURKINA FASO.

 

Kapteni Ibrahim Traoré alichukua madaraka miaka mitatu iliyopita

Utawala wa kijeshi wa Burkina Faso umevunjalia mbali tume ya uchaguzi nchini humo ukiitaja kuwa ni ufujaji wa fedha.

Badala yake wizara ya mambo ya ndani itashughulikia uchaguzi katika siku zijazo, runinga ya serikali ya RTB iliripoti.

Tangu utawala huo ulipoingia mamlaka mnamo Septemba 2022, viongozi wake mapinduzi wameanzisha mageuzi makubwa, ikiwa ni pamoja na kuahirishwa kwa uchaguzi ambao ungesababisha kurejea kwa utawala wa kiraia.

Uchaguzi mkuu ilitarajiwa kufanyika mwaka jana, lakini serikali ya kijeshi iliongeza muda wa mpito kwa demokrasia hadi Julai 2029, na kumruhusu kiongozi Kapteni Ibrahim Traoré kusalia madarakani na kuwa huru kugombea uchaguzi ujao wa urais.

Shirika la habari la AFP linamnukuu Waziri wa Utawala wa Wilaya Emile Zerbo akisema kwamba tume ya uchaguzi "iligharimu" seriklai takriban dola 870,000 kwa mwaka.

Kufuta tume hiyo "kutaimarisha udhibiti wetu wa mchakato wa uchaguzi na wakati huo huo kupunguza ushawishi wa kigeni", aliongeza.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI