Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), akizindua rasmi Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini (Government Enterprise Service Bus - GovESB) kwa kutumia kishkwambi, katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2025, katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Mfumo wa GovESB umesanifiwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao(e-GA) ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Tanzania Mh.Dkt.Samia Suluhu Hassan na Sheria ya Serikali Mtandao Namba 10, ya mwaka 2019, ya kuhakikisha mifumo yote ya taasisi za umma inasoma na kubadilishana taarifa, ili kuboresha huduma kwa wananchi.
0 Comments