Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu akitembelea eneo la Israel lililoshambuliwa na makombora ya Iran
Mwezi Machi, alipoupa kisogo mchakato wa kusitisha mapigano uliokuwa ukitoa matokeo, waziri mkuu wa Israel alichukua uamuzi ulioelezewa na baadhi ya wachambuzi kuwa ni sawa na "kujiua kisiasa".
Makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza, yaliyosimamiwa na mjumbe wa Donald Trump Steve Witkoff hata kabla ya rais wa Marekani kuapishwa kwa muhula wake wa pili, yalisababisha kuachiliwa kwa makumi ya mateka kutoka utumwa wa Hamas, badala ya mamia ya wafungwa wa Kipalestina kutoka jela za Israel.
Hatua iliyofuata ilitokana na kuona mateka zaidi wakirejea nyumbani na kuondolewa taratibu kwa wanajeshi wa Israel kutoka Gaza, kabla ya kumalizika kwa mazungumzo kwa vita.
Wakiwa wamechoshwa na mzozo, Waisrael na Wapalestina walitafakari mwisho wa vita haribifu zaidi katika historia ya vita ambavyo vimekuwa vya kawaida kwao.
Lakini Benjamin Netanyahu hakutaka vita viishe.
Alipoamuru kuanza kwa mashambulizi kote Gaza, waziri mkuu alitangaza kwamba mapigano yataendelea hadi Hamas "imeangamizwa kabisa".
Kurudi salama kwa mateka waliosalia huko Gaza kulionekana kuwa jambo la pili. (Madhara ya raia huko Gaza yenyewe hayakustahili kutajwa.)
Waisraeli wengi, hasa familia za mateka, walikuwa na hasira.
Walimshutumu Netanyahu kwa kuweka uhai wake wa kisiasa mbele ya usalama wa jamaa zao na manufaa makubwa ya taifa.
Umaarufu wake katika kura za maoni ulishuka na alijitahidi kuiweka pamoja serikali isiyoungana, ikiungwa mkono na mawaziri wenye misimamo mikali kutoka vyama vya mrengo wa kulia na vya kidini.
Miezi mitatu baadaye, Netanyahu anafurahia ushindi wa ajabu wa kijeshi dhidi ya adui yake, Iran. Sasa anasemekana kutafakari uchaguzi wa mapema na muhula mwingine kama waziri mkuu.
0 Comments