Mahakama Kuu imetangaza kusitisha agizo la Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CA) la kupiga marufuku vituo vyote vya runinga na redio kurusha matangazo ya moja kwa moja ya maandamano, na kwamba kituo chochote kilichozimwa kutokana na agizo hilo kirejeshwe hewani mara moja
Jaji Chacha Mwita, ameagiza vituo vya NTV, KTN na K24 kurejeshwa hewani kutokana na ombi lililowasilishwa na Chama cha Wanasheria wa Kenya (LSK) na Chama cha Wahariri wa Kenya (KEG) kuhusu hatua iliyochukuliwa na Serikali
Matangazo ya vituo hivyo yalizimwa wakati kukiwa na maandamano makubwa ya kitaifa dhidi ya Serikali, kuadhimisha Mwaka mmoja tangu maandamano ya Juni 25, 2024 ya Vijana ya kupinga muswada wa fedha, yaliyogharimu maisha ya takriban Watu 60
0 Comments