Header Ads Widget

WASHIKILIWA KWA MAUAJI MORO,MMOJA AMUUA BABA AKE MZAZI MWINGINE WIVU WA MAPENZI

 

Na Lilian Kasenene,Morogoro

Jeshi  la polisi mkoa wa Morogoro  linawashikilia watu  wawili kwa tuhuma  za mauaji  katika matukio tofauti yaliotokea huko  Ruhembe wilayani Kilosa.

Kamanda wa polisi mkoani Morogoro  Alex Mkama alisema  tukio la kwanza limetokea Mei 26 mwaka huu katika kijiji cha Simbalambende  kata ya Ruaha  wilayani Kilosa.

Kamanda huyo alimtaja Said  Kandulu  (52) mkazi wa  Simbalambende  alifariki dunia baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali  eneo la kifuani  upande wa kushoto.

Alimtaja mtuhumiwa wa tukio hilo kuwa ni Lucas  Zacharia  Kanyenze (64) mkazi wa  Hyamvisi ambapo alisema chanzo cha tukio hilo ni  wivu wa kimapenzi .

"Marehemu  alikuwa anamtuhumu mtuhumiwa kuwa kamuoa mtalaka wake ,ugomvi huo ulichochewa na ulevi"alisema.

Katika tukio la pili jeshi la polisi mkoani hapa linamshikilia Ayubu Rashid Ayubu (23) mkazi wa Gang'anda  kwa tuhuma za kumuua baba yake  mzazi .

Alisema tukio hilo limetokea  Mei 29 mwaka huu majira ya Asubuhi katika kitongoji cha Gang'anda, kijiji cha Mfuru, kata ya Tegetero wilayani Morogoro. 

Kamanda huyo alimtaja Rashid Ayubu Juma (71) mkazi wa  Gang'anda alikufa kwa kushambuliwa na panga eneo la kichwani  upande wa kisogoni  na mwanae  wakati  marehemu  akiwa amepumzika nyumbani kwake.

Alisema  kijana huyo ghafla alianza kumshambulia kisogoni mithiri ya kukata mti na kusababisha  kupoteza maisha  na kwamba mtuhumiwa amekamatwa ambapo alisema chanzo cha tukio hilo ni matatizo ya Afya ya akili.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI