Header Ads Widget

VIJANA 26 KUSHIRIKI PROGRAMS YA MANDELA WASHINGTON FELLOWSHIP 2025 NCHINI MAREKANI


Vijana waliochaguliwa kushiriki progranu ya Mandela Washington Fellowship kwa mwaka 2025, wamekumbushwa kuwa fursa waliyoipata haikuja kwa bahati, isipokuwa kutokana na majukumu wanayoyafanya ambayo yana mchango mkubwa kwa jamii.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa wakati anawapa nasaha za kuwaaga vijana hao 26 jijini Dodoma Mei 30, 2025.

Balozi Mussa aliwataka kutumia fursa hiyo kujifunza mambo mapya kwa kuwa nchi wanayokwenda imeendelea kiuchumi na kiteknolojia duniani na itawapa fursa pia ya kukutana na raia wa mataifa mbalimbali wenye uzoefu na mila tofauti.

Vijana hao ambao wanatarajiwa kwenda nchini Marekani Juni na kurejea Agosti 2025,  wametakiwa kulitangaza jina la Tanzania kwa watu watakaokutana nao. "Mtalitangaza jina la nchi yetu kwa kuheshimu sheria za nchi mnayokwenda,  kutangaza utamaduni mzuri wa Tanzania na kuelezea kwa ufasaha mambo makubwa na mazuri ya nchi kama vile mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama, maziwa, mito na maendeleo ya miundombinu", Balozi Mussa alisema. 

Balozi Mussa alisema kuwa kuwepo kwao katika programu hiyo ni kielezo cha uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Marekani ambao umedumu tokea ulipoanzishwa mwaka 1961.

Pogranu ya Mandela Washington Fellowship ilizinduliwa mwaka 2014 na hadi sasa vijana 6500 kutoka nchi za Afrika wamefaidika na mpango huo ambao unalenga kuwajengea uwezo vijana, kupata mbinu na ujuzi wa uongozi utakaosaidia kuleta mabadiliko chanya ya kiuchumi, kisiasa na kijamii barani Afrika.



 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI