Header Ads Widget

WANAJESHI WA ISRAEL WAPINGA VITA DHIDI YA GAZA

 

Katika wiki za hivi karibuni, maelfu ya askari wa akiba wa Israel - kutoka matawi yote ya jeshi - wametia saini barua wakiitaka serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kusitisha mapigano na kujikita zaidi katika kufikia makubaliano ya kuwarudisha mateka 59 waliosalia wanaoshikiliwa na Hamas.

Miezi kumi na minane iliyopita, Waisrael wachache walitilia shaka mantiki ya vita: kuwashinda Hamas na kuwarudisha mateka.

Kwa wengi, usitishaji vita wa Januari na kurudi kwa mateka zaidi ya 30 kuliweka matumaini kwamba vita vinaweza kuisha hivi karibuni.

Lakini baada ya Israel kurejea vitani katikati ya mwezi Machi, matumaini hayo yalikatizwa.

"Tulifikia hitimisho kwamba Israel inaenda mahali pabaya sana," Danny Yatom, mkuu wa zamani wa shirika la kijasusi la Mossad alisema.

"Tunaelewa kwamba kinachomsumbua zaidi Netanyahu ni maslahi yake mwenyewe. Na katika orodha ya vipaumbele, maslahi yake na maslahi ya kuwa na serikali imara ndiyo ya kwanza, na sio mateka."

Wengi wa wale wanaotia saini barua za hivi majuzi ni, kama Yatom, wakosoaji wa muda mrefu wa waziri mkuu. Baadhi walihusika katika maandamano ya kuipinga serikali yaliyotangulia kuzuka kwa vita tarehe 7 Oktoba 2023 kufuatia mashambulizi ya Hamas dhidi ya Israel.

Lakini Yatom anasema hiyo sio sababu ya kuamua kuzungumza.

"Nilisaini jina langu na ninashiriki maandamano si kwa sababu yoyote ya kisiasa, lakini kwa sababu ya kitaifa," alisema.

"Nina wasiwasi sana kwamba nchi yangu itapoteza mwelekeo."

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI