Mfumo wa haki za jeshi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, umetuma ombi rasmi kwa bunge la Seneti kuomba kuondolewa kwa kinga ya Joseph Kabila.
Rais wa zamani, sasa ni seneta wa kudumu, anashukiwa kuwa na uhusiano na Congo River Alliance, muungano wa makundi ya waasi.
Anashtakiwa kwa uhaini, uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya binadamu, na kushiriki katika harakati za uchochezi.
Mfumo wa haki za kijeshi unaangazia hadhi ya Joseph Kabila kama seneta wa kudumu kuanzisha kesi hiyo.
Vitendo hivyo vinadaiwa kutokea baada ya muda wake wa urais. Waziri wa Sheria Constant Mutamba anasema kwamba ushahidi huo upo sasa.
"Mfumo wa Sheria imekusanya ushahidi mwingi uliowazi na usioweza kukanushwa ambao unaonyesha wazi kuhusika kwa Seneta wa kudumu Joseph Kabila Kabange katika uhalifu wa vita, uhalifu dhidi ya ubinadamu, na mauaji ya raia, raia wa kawaida na wanajeshi katika sehemu ya mashariki ya nchi kwa sasa. Tunamkaribisha kiongozi huyo wa zamani serikalini kuja na kukabiliana na mfumo wa haki wa Congo", Waziri wa Sheria wa Congo alitangaza Jumatano, Aprili 30.
Chama cha Joseph Kabila, kilichosimamishwa na serikali, kinakanusha madai hayo.
Kwa wiki kadhaa, imekuwa ikiyataja madai ya uwongo.
0 Comments