Na Hamida Ramadhan, Matukio Daima App Dodoma
Wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Dodoma wameamua kuacha kuwa watazamaji wa vitendo vya uhalifu kwenye taasisi zao na badala yake wamechukua hatua—kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani humo, kuweka mikakati ya pamoja ya kuhakikisha usalama wao chuoni.
Katika kikao kilichowakutanisha na polisi mnamo Mei 15, 2025, viongozi wa serikali za wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali walijadili mbinu mpya za kupambana na changamoto kama ukatili wa kijinsia, wizi wa kimtandao, mahusiano hatarishi, na mitindo ya maisha inayohatarisha usalama wa wanafunzi.
Wakizungumza kwa niaba ya wenzao, baadhi ya viongozi walipendekeza kuanzishwa kwa klabu za uhamasishaji wa amani na maadili chuoni, kushirikiana na polisi katika kutoa elimu ya sheria kwa wanafunzi wapya, pamoja na kuanzisha vikundi vya ulinzi wa ndani vya kujitolea.
“Tunatambua hatuwezi kukaa kimya wakati uhalifu unatuathiri sisi moja kwa moja. Tunahitaji kuwa sehemu ya suluhisho,” alisema mmoja wa viongozi wa wanafunzi.
0 Comments