Header Ads Widget

TRAORE ASHUKURU NCHI ZILIZOANDAMANA KUMUUNGA MKONO

 

Kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Burkina Faso, Kapteni Ibrahim Traoré, ametoa shukurani zake za dhati kwa nchi zilizoandamana duniani kote jana Jumatano, akisema mshikamano huo umeimarisha imani yao kwamba mapigano wanayopigania ni kupatikana kwa ulimwengu mzuri na usawa zaidi na wenye haki.

"Napenda kutoa shukrani zangu kwa wazalendo wote wanaopenda amani, wapenda uhuru na wapendelea Afrika wote ambao waliandamana ulimwenguni kote Jumatano Aprili 30, 2025 kuunga mkono kujitolea kwetu na maono yetu ya Burkina Faso mpya na Afrika mpya, kujiweka huru kutoka kwa mikono ya ubeberu na ukoloni," Traore aliandika katika akaunti yake ya X.

Aliahidi kutobadilisha msimamo hata wakati anapopitia changamoto, badala yake "nitasimama kidete hadi watu wetu watakapokombolewa."

Maelfu ya raia barani kote Afrika kote waliandamana chini ya wito wa "Hands Off the AES!" kuonyesha mshikamano wao na Burkina Faso na kiongozi wake wa kijeshi, Kapteni Ibrahim Traoré.

Maandamano yalifanyika Burkina Faso, Ghana, na Liberia na kwengine yakiongozwa na mashirika ya mashinani.

Waandamanaji walilaani vikali uingiliaji wa mataifa ya kigeni na kusisitiza kuunga mkono nchi hiyo dhidi ya ubeberu.

Wimbi hili la mshikamano barani Afrika linafuatia ufichuzi wa hivi majuzi wa mamlaka ya kijeshi ya Burkina Faso kwamba ilizima "njama kubwa" ya kumpindua Traore Aprili 21.

Serikali ya Burkina Faso ilielezea njama hiyo kama juhudi ya "kuzua machafuko" na kubadilisha utawala chini ya uongozi wa Traoré.

"Chini ya Kapteni Traoré, Burkina Faso imekuwa ishara ya utu na ukakamavu wa Afrika," lilisema Vuguvugu la Kisoshalisti la Ghana ambalo liliandaa maandamano nchini Ghana.

"Tunasimama na watu wa Burkina Faso ambao wanapigania kurejesha utajiri wao na mustakabali wao kutoka kwenye makucha ya ukoloni mamboleo."

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI