Kanali wa Jeshi la India Sofiya Qureshi, ameishutumu Pakistan kwa kutumia makombora ya masafa marefu kulenga vituo vya anga vya India.
Taarifa hiyo imetolewa saa chache baada ya Pakistan kuishutumu India kwa kulenga vituo vyake vitatu vya kijeshi kwa mashambulizi ya makombora.
Wakiwa katika mkutano, Waziri wa Mambo ya Nje wa India Vikram Misri anawaambia waliokusanyika:
"Nimesema katika matukio mengi ya awali, hatua za Pakistani ndio ambazo zimesababisha uchochezi na kuongezeka kwa mzozo huu.
Kamanda wa Jeshi la Wanahewa la India Vyomika Singh, amesema Pakistan ilifanya "vitendo vikali kwa kutumia vienezaji vingi vya vitisho" kuzunguka mpaka wa magharibi wa India.
Amesema Pakistan ilitumia silaha - ikiwa ni pamoja na ndege zisizo na rubani na makombora ya masafa marefu - "kulenga raia na miundombinu ya kijeshi".
"Ikijibu, India imejitetea ikisema imechukua hatua zenye kipimo na kuwajibika kutokana na uchochezi unaoongezeka kutoka upande wa Pakistani.
"Mapema asubuhi ya leo, kumekuwa na marudio ya vitendo vya uchokozi."
0 Comments