Header Ads Widget

INDIA IKO KATIKA HALI YA TAHADHARI BAADA YA MELI ILIYOBEBA SHEHENA HATARI KUZAMA

Mamlaka katika jimbo la Kerala kusini mwa India wametoa tahadhari baada ya meli iliyokuwa imebeba mafuta na shehena ya hatari kuvuja na kuzama katika ufuo wa jimbo hilo katika bahari ya Arabia.

Mwagikaji huo ulitokea katika meli yenye bendera ya Liberia ambayo ilipinduka karibu na jiji la Kochi siku ya Jumapili.

Ukanda wa pwani una wingi wa viumbe hai na pia ni kivutio muhimu cha watalii.

Wafanyakazi wote 24 waliokuwemo kwenye meli hiyo wameokolewa lakini baadhi ya makontena 640 ya meli hiyo yameripotiwa kuwa yakielea ufukweni na hivyo kusababisha yahamishwe.

Mamlaka inahofia kuwa mafuta, fyueli na vitu vingine vyenye madhara ambavyo vimevuja kutoka kwa meli na shehena yake vinaweza kuhatarisha afya ya wakaazi na viumbe vya baharini.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI