Header Ads Widget

WAZIRI WA ULINZI WA UINGEREZA AKUTANA NA FAMILIA YA AGNES WANJIRU ALIYEUAWA KENYA

 



Waziri wa Ulinzi wa Uingereza, John Healey MP, leo amekutana na familia ya Agnes Wanjiru, ambaye aliuawa kikatili huko Nanyuki, Kenya, mwaka 2012, ili kutoa rambirambi zake na kutimiza ahadi aliyotoa aliposhika wadhifa huo.

Huu ni mkutano wa kwanza kwa Waziri wa Serikali ya Uingereza na familia ya Agnes Wanjiru.

Waziri Healey alisema: “Ilikuwa ni heshima kubwa kukutana na familia ya Agnes Wanjiru leo. Katika miaka 13 tangu kifo chake, familia imeonyesha nguvu na uvumilivu mkubwa katika vita yao ya kudai haki''.

Aidha ameeleza dhmira yake ya kuhakikisha kesi hii imetatuliwa huku akikiri kukutana na Rais wa Kenya William Ruto.

“Tutazidi kutoa msaada wetu kamili kwa mamlaka za uchunguzi za Kenya, ikiwa ni pamoja na ziara za wachunguzi wa Kenya nchini Uingereza kuhoji mashahidi, na pia ziara ya maafisa wa uhalifu mkubwa kwenda Kenya'', waziri huyo alisema.

Familia ya Agnes Wanjiru pia ilitoa tamko baada ya mkutano na Waziri Healey.

“Kifo cha mpendwa wetu Agnes kimeleta maumivu makubwa na athari za kudumu katika familia yetu. Haikuwa tu mshtuko wa kumpoteza Agnes akiwa na umri mdogo, bali pia hali ya kutisha ambayo mwili wake ulipatikana na machungu yote ambayo familia yetu imepitia katika kutafuta haki na uwajibikaji kwa kifo chake, yaliyosababisha mateso makubwa kwa kila mmoja wetu'', familia yasema.

Mkutano huu unajiri baada ya miaka 13 tangu Agnes auawe, na karibu miaka 6 tangu uchunguzi wa Kenya kugundua kuwa aliuawa na wanajeshi wa Uingereza, lakini bado hakuna maendeleo makubwa yaliyopatikana tangu wakati huo.

“Tunashukuru kwa Waziri wa Ulinzi kukubali kukutana nasi, lakini tumekaa kwa miaka mingi tukiahidiwa ahadi zisizotekelezwa. Tunatumai kwamba mkutano wetu na Waziri wa Ulinzi utakuwa mwanzo wa hatua madhubuti kutoka kwa Serikali ya Uingereza na Wizara ya Ulinzi kuhakikisha kuwa kilichotokea kwa Agnes kinachunguzwa kwa kina, si tu Kenya bali pia Uingereza, na kwamba hakutatokea tena''.

Waliohudhuria mkutano ni pamoja na Kamishna Mkuu wa Uingereza nchini Kenya, Neil Wigan, ambaye ameendelea kuhusika kikamilifu na familia ya Bi. Wanjiru.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI